Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA SUNGURA NA VYURA

Sungura walikuwa wakionewa sana na wanyama wengine kwa kupigwa, kuwindwa na kuliwa, kiasi kwamba hawakujua wakimbilie wapi. Ikawa wanaishi maisha ya karaha mno na kila walipomwona mnyama yeyote akiwakaribia, walilazimika kutimua mbio kwa woga.
Siku moja wakaliona kundi la Farasi pori walio katika hali ya taharuki wakikimbia na kuwaelekea wao. Walihamaki na kutimka kuelekea ziwani, wakiwa na nia ya kujitupa majini ili wafe, kwani waliona ni heri kufa kuliko kuendelea kuishi katika adha na karaha ile ya kunyanyaswa, na maisha ya roho mkononi.

Lakini walipokaribia kingo za ziwa, kundi la Chura waliokuwa wamejipumzisha wakitafakari, walishtushwa sana na vishindo vya Sungura hao, nao walitaharuki wakageuka kwa woga na kujitupa ziwani kuokoa maisha yao.
Kwa kweli,” alisema mmoja wa Sungura, “kumbe hali yetu sisi siyo mbaya sana kama tunavyodhani.”
Share:

Maoni 3 :

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu