Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA KIJANA NA UPUPU

Hapo zamani kulikuwa na Kijana mmoja mtukutu ambaye alipenda sana kuchezea mimea na wadudu. Siku moja akiwa kwenye kichaka jirani na nyumbani kwake, aligusa Upupu kwa mkono wake wa kuume, nao ukaanza kumwasha. Ukamletea karaha na maumivu makali.

Akaamua kukimbilia nyumbani kwake haraka huku akiendelea kujikuna na machozi yakimlengalenga. Alimfuata Mama yake bustanini na kumwambia kwa sauti ya kudeka akisema,
Mama, Ingawa upupu unanichomachoma na kuniletea maumivu makali kiasi hiki, mie niliugusa taratibu na kwa unyenyekevu. Sijui ni kwa nini unaniumiza hivi”
Kuugusa taratibu ndiyo haswa sababu iliyopelekea ukuchome, na kukuumiza.” Mama yake alimwambia. “Siku nyingine mwanangu, ukitaka kuugusa Upupu, ukamate na uufinye kwa nguvu, nao utakuwa laini na mororo kiganjani mwako, na wala hautokuchoma na kukuumiza hata kidogo.”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu