Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA KIJANA MWINDA SENENE

Kijana mmoja mdogo alikuwa akidaka Senene kwenye majani yaliyomea kando ya shamba lao. Ilikuwa ni mapema wakati wa asubuhi, hata umande ungali haujavukizwa. Baada ya nusu saa tu alifanikiwa kuwadaka Senene wengi sana. Wakati akijiandaa kurudi nyumbani, alitupa macho huku na huko na kumwona Nge akiwa amejipachika katikati ya majani mawili. Basi yule Kijana kwa haraka yake hakuweza kutambua kuwa yule ni Nge na badala yake alimfananisha na Senene. Akanyoosha mkono wake ili amkamate, aongezee idadi ya kitoweo.

Nge naye akaunyoosha mwiba wake tayari kwa kung’ata na kumuasa yule Kijana, akasema;
ee Kijana mwenye uchu na ulafi, laiti ungelithubutu hata kunigusa tu, ungejuta, kwani ungelinikosa mimi na pia hao Senene wote uliokwisha kuwapata!”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu