Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MWANAMFALME NA PICHA YA SIMBA

Hapo zamani kulikuwako Mfalme, ambaye alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume, kijana aliyependa sana mazoezi ya sanaa za mapigano. Kila siku alijichanganya na vijana wa rika lake katika mazoezi na michezo. Na awapo nyumbani alipendwa sana na wazazi wake, hasa baba yake.

Siku moja Mfalme akiwa usingizini aliota ndoto. Na katika ndoto hiyo alipewa onyo la kuwa mwanaye huyo wa pekee atakufa kwa kuuawa na kuliwa na Simba.
Aliposhtuka alipatwa na hofu, kwani katika himaya yake wanyama wakali kama Simba kushambulia binadamu au mifugo ilikuwa kawaida.
Kwa kuhofia huenda ndoto yake ikawa ni ujumbe wa kweli, aliamua kumjengea yule mwanaye, Mwanamfalme, kasri kubwa maridadi.

Jengo lilinakshiwa maridadi na kuta zote zilipambwa kwa picha nzuri za wanyama mbalimbali, zikiwa na ukubwa unaolingana na wa wanyama halisi. Mojawapo kati ya zile picha za ukutani ilikuwa ni picha ya Simba dume.
Hivyo Mwanamfalme aliwekwa ndani ya kasri, akapewa mahitaji yote humo, akafungiwa asitoke nje hata mara moja kwa hofu ya kuuawa na Simba.

Siku moja yule kijana mwana wa mfalme aliiona ile picha ya Simba, ndipo huzuni yake ya kukosa uhuru na kufungiwa ikafufuka upya, na akiwa amesimama kando ya ile picha ya Simba, aliitazama kwa jazba na kusema: “ee mnyama ninayekuchukia kuliko wanyama wote! Kutokana na ndoto ya uwongo aliyoota baba yangu, na kuona maono ya usingizini, nimefungiwa ndani ya kasri hili kama mtoto wa kike, nisitoke kwa kukuhofia wewe: nikutende nini sasa baradhuli mkubwa wee?” Akisema hivyo aliunyoosha mkono wake wa kuume kuelekea mti wa miiba, kwa nia ya kukata tawi atengeneze fimbo ili amsulubu yule Simba kwa kisasi.

Bahati mbaya miba moja ilimchoma kidoleni, akatokwa damu nyingi na kupata maumivu makali sana, kiasi kwamba Mwanamfalme alianguka chini na kuzirai. Ghafla alishikwa na homa kali, ambayo ilimuua siku chache baadaye.

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu