Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA SUNGURA NA MBWEHA

Hapo zamani za kale Sungura walianzisha vita na Tai. Mapambano yalianza na kila upande ukijigamba na kudhani ulikuwa na uwezo wa kumshinda mwenzie.

Vita vilipopamba moto, Sungura walihisi kuzidiwa. Baada ya vikao na mashauriano ya majemedari, walikubaliana kutuma maombi kwa Mbweha ili waje kama mamluki kuwasaidia kupambana na jeshi shupavu la Tai.

Mbweha wakajibu, “tungeweza kuja kuwasaidia kwa moyo mmoja, iwapo tusingeliwafahamu ninyi ni nani, na ni nani hao mnaopigana nao vita.”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu