Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA BABU KIZEE NA KIFO

Babu kizee mmoja aliajiriwa kufanya kazi ya kukata magogo ya miti msituni. Siku moja akiwa anarejea nyumbani jioni alibebeshwa mzigo wa kuni aupeleke mjini ukauzwe. Mzigo ule ulikuwa mzito sana kwake.
Baada ya mwendo wa kitambo kirefu alichoka akawa hoi kabisa. Alisononeka kwa ufukara wake unaopelekea apate mateso ya kufanya kazi mzito mchana kutwa, na jioni kutwikwa mizigo mizito katika umri kama ule.
Mwishowe aliamua kuutupa chini mzigo ule, akaketi kando ya njia, akajiinamia na kuomba kwa dhati kabisa “Kifo” kimchukue aepuke suluba na mateso ya kubeba mzigo ule.
Kwa bahati nzuri ombi lake lilisikika na kutekelezwa bila ucheleweshaji; alipoinua uso wake baada ya kumaliza kuomba, alimwona “Kifo” amesimama mbele yake tayari kwa kazi, akiwa amekuja kuitika ule wito wake.
Kifo akauliza, “nimesikia wito wako ee mzee, je unataka nini hata ukaniita nikujie?”
Mzee akajibu haraka, “nilihitaji unipe msaada wa kuuinua mzigo huu wa kuni, unitwike mabegani kwangu niendelee na safari.”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu