Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumamosi, 21 Desemba 2013

KISA CHA MJAKAZI NA NYOKA

Hapo zamani za kale, kulikuwapo Nyoka mkubwa mwenye sumu kali, ambaye aliweka makazi yake kwenye shimo pembezoni mwa baraza ya nyumba ya Mjakazi mmoja. Siku moja usiku wa manane yule Nyoka alimng’ata mtoto mchanga wa Mjakazi, mwili wake ukabadilika rangi kuwa mweusi tii, akafa.
Kukawa msiba na simanzi isiyo kifani.
Wakati akiomboleza kifo cha mwanae kwa uchungu, mtu huyo aliapa kulipiza kisasi kwa kumuua Nyoka huyo pindi atakapopata wasaa.
Siku iliyofuata, majira ya jioni, Nyoka yule alitoka shimoni ili kwenda kujitafutia chakula. Ndipo Mjakazi alimwona akitambaa kwenye kiambaza kuelekea ndani, akachukua shoka na kumwendea kwa hasira ili ammalize. Na kwa kuwa
alinyanyua shoka na kutaka kumshambulia kwa papara, alikikosa kichwa na kiwiliwili na badala yake akamkata ncha ya mkia tu.
Nyoka akafanikiwa kujiokoa na kurudi ndani ya shimo.
Baada ya siku kadhaa kupita, Mjakazi yule akalemewa na hofu ya kuwa yeye pia yu hatarini kung’atwa na yule Nyoka. Akapata wazo la kuanzisha mchakato wa kumrubuni nyoka waafikiane kuishi kwa amani. Akamtengea mikate na chumvi kando ya shimo lake, na maji ya kunywa, ikiwa ni ishara ya kuomba urafiki.
Yule nyoka, huku akitoa mlio wa tahadhari na kitisho, alimwambia: “ndugu, kamwe hakuwezi kuwa na amani ya kweli kati yako nami; kwani kila nitakapokuona nitakumbuka nilivyopoteza mkia wangu, nawe kila unionapo utakumbuka kifo cha mwanao.”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu