Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatano, 28 Februari 2018

Kisa cha Beberu Wawili

    Mbuzi wawili Beberu walikuwa wakirandaranda kwenye pande mbili za mlima kila mmoja kivyake. Kwa bahati mbaya walikutana kwenye eneo lenye korongo lenye kina kirefu sana ambalo chini yake kulikuwa na mto mkubwa uliotiririka kwa kasi.
    Tawi la mti ulioanguka lilikatiza juu ya korongo hilo na ndo lilikuwa njia pekee ya kuweza kuvuka, na juu ya tawi hilo hata panya buku wawili wasingaliweza kupita kwa pamoja salama. Kwa jinsi njia hiyo ilivyokuwa nyembamba kulinganisha na ukubwa wa korongo, hata kiumbe jasiri vipi angalitetemeka kwa woga.
    Lakini si kwa Beberu wale. Kwa tabia yao ya kiburi na kupenda kujikweza, hakuna mmoja kati yao aliyekuwa tayari kumpisha mwenzie avuke kwanza.
    Basi ikawa, Beberu mmoja alikita miguu kibabe kwenye gogo. Na mwingine naye akafanya vivyo hivyo. Katikati waliinamisha vichwa wakaumanisha pembe zao. Hivyo walianza kusukumana na hatimaye wote walianguka korongoni wakasombwa na maji na kuangamia.

Mwisho
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu