Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumamosi, 21 Desemba 2013

KISA CHA NGURUWE, KONDOO NA MBUZI

Nguruwe mmoja mdogo alikuwa amefungiwa kwenye uzio wa miti. Mbuzi na Kondoo pia walifungwa pamoja naye. Siku moja Mchungaji wao alikuja na kumkamata yule Nguruwe, ambaye aliguna na kuanza kupiga kelele na kufurukuta.
Mbuzi na Kondoo walimlalamikia Nguruwe kwa kelele zake za kilio na purukushani, wakasema kwa kejeli, “Mara kwa mara Mchungaji wetu hutushika sisi, na hatuangui kilio kama yeye.”
Kusikia hivyo, Nguruwe akawajibu, “Mchungaji anavyowashika ninyi na anavyonishika mimi ni vitu viwili tofauti kabisa. Kwani anapowashika ninyi huhitaji kutoka kwenu sufu na maziwa tu, lakini anaponishika mimi ana nia ya kunipokonya uhai wangu.”
Hadithi hii inatufundisha nini?
 
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;


Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu