Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MBUZI NA MCHUNGAJI

Mchunga Mbuzi alihangaika kumrudisha Mbuzi mmoja aliyetoka kundini na kuingia kwenye shamba la jirani. Alipiga mbinja na kupuliza baragumu bila ya mafanikio; yule Mbuzi alimbeza na kuidharau miito yote. Mwishowe Mchunga Mbuzi aliudhika na kumrushia jiwe kwa nguvu, likamvunja pembe moja.

Kuona vile Mchunga Mbuzi alipagawa kwa huruma na hofu. Alimbembeleza yule Mbuzi kwamba watakaporejea nyumbani asimdondolee bwana mwenye mbuzi kilichosibu. Mbuzi akamjibu, “Kivipi ewe Mchunga mpumbavu, hujui kuwa hata nikifunga mdomo wangu, pembe yenyewe itaongea!”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu