Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Alhamisi, 1 Machi 2018

Mbweha na Beberu



Siku moja Mbweha alitumbukia kisimani kwa bahati mbaya, na ingawa kisima chenyewe hakikuwa na kina kirefu sana, alijikuta akishindwa kutoka nje tena. Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, hatimaye akatokea Beberu mwenye kiu kali. Beberu alidhani kuwa Mbweha ametumbukia kwenda kunywa maji kukidhi kiu yake, na hivyo akauliza kama maji yalikuwa safi au la.

“Ni safi na matamu kupita maji yote kwenye nchi hii,” alijibu Mbweha yule mjanja, “jirushe utumbukie ujionee mwenyewe. Maji ni mengi yanatutosha sote na tutasaza.”

Beberu mwenye kiu mara moja alijitosa kisimani na kuanza kuyafakami maji. Mbweha naye kwa haraka sana alimdandia Beberu mgongoni akachupa kwenye ncha za pembe za Beberu na kutoka zake nje ya kisima.
Yule Beberu mpumbavu akang’amua kuwa amejiingiza matatizoni, akaanza kumbembeleza Mbweha amsaidie kumtoa kisimani. Lakini Mbweha tayari alikwishaanza kutokomea zake mitini.

“Laiti ungalikuwa na akili kama ulivyo na ndevu, rafiki,” alimwambia huku akikimbia zake, “ungalikuwa makini na kujaribu kung’amua kwanza njia utakayoitumia kutokea kisimani kabla hujatumbukia.”

Mwisho.
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu