Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MBWEHA NA MBU

Siku moja, baada ya kutembea kwa muda mrefu, Mbweha aliukuta mto mdogo wenye kina kifupi cha maji. Maji yalikuwa masafi na maangavu kabisa na mandhari ya bonde lile kwa ujumla ilikuwa ya kuvutia kutokana na uoto na magugu yaliyonawiri vizuri pembezoni. Akayatamani maji kwa uzuri wake japo hakuwa na kiu kabla, akayanywa, kisha akatulia kidogo kwa tafakuri.

Hapohapo akapata wazo la kwenda ng’ambo ya mto kumtembelea rafiki yake ambaye hawakuwahi kuonana kwa takribani miezi kenda. Na kwa kuwa ilikuwa muda wa jioni aliona ni vyema zaidi kwani katika mila za kimbweha, kulala kwa rafiki huchukuliwa kama heshima kubwa na ishara ya urafiki wa kweli. Akajitoma majini na kuvuka.
 
Baada ya kufika ng’ambo ya mto Mbweha alijikuta akiunasisha mkia wake kwenye magugu kizembe, na kila alivyofanya jitihada za kujinasua ndo kwanza alijinasisha zaidi. Mwisho akawa hana uwezo wa kwenda wala kusogea.
Kundi la Mbu lilipita eneo lile na kuona tatizo lililomkabili, wakashauriana na kutua wote kwa pamoja kwenye mwili wake, wakamnyonya na kujipatia mlo wa damu pasipo bughudha ya mkia wake.

Nungunungu, akiwa hana hili wala lile, naye akapita mahali pale na kuona matatizo mawili yanayomkabili Mbweha. Alimhurumia sana, akamfuata na kumwambia: “Pole ee jirani yangu, naona upo kwenye mapitio mabaya, je nikusaidie kupunguza maswaibu yako kwa kuwafukuza hao Mbu wakunyonyao damu yako?”
Mbweha aliguna na kumjibu,

Asante sana kwa kunijali na kwa nia yako ya kutaka kunitatulia tatizo moja kati ya mawili haya, rafiki Nungunungu,” alisema, “ila naona ni heri usiwafukuze hawa Mbu.”
Kwa nini, wanakutesa na kukunyonya halafu hutaki niwaondoe!?”
Sikiliza rafiki,” alijibu Mbweha, “Mbu hawa wameninyonya sana na kwa sasa wamekwishashiba, matumbo yao yamejaa damu yangu; endapo utawafukuza hawa, Mbu wengine wenye njaa kali watakuja kuchukua nafasi yao, waninyonye upya na pengine kuniua kabisa.”
ibot.isk@gmail.com  
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu