Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

HADITHI YA MTU NA MTI

Mtu mmoja alikwenda kichakani huku akiwa na shoka mikononi kwake, na kuiomba Miti kwa unyenyekevu ili iweze kumpa tawi moja tu dogo ambalo alisema alikuwa na kazi nalo fulani.

Miti ile ilikuwa na tabia njema, ikampa moja ya matawi yake. Kumbe yule mtu alikuwa akihitaji mpini wa shoka lake. Kwa kutumia tawi lile alilopewa akakarabati shoka lake na kisha kuanza kazi ya kuikata Miti ile mmoja baada ya mwingine.

Ndipo Miti ilipon’gamua ilitenda ujinga kwa kiasi gani kutokana na kitendo kile cha kumsaidia adui yao mpini, ambao ulitumika kulitengeneza shoka, ambalo lilitumika kuiangamiza Miti yenyewe.

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu