Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA SUNGURA NA MBWA

Katika pitapita zake za mawindo, Mbwa alimvumbua Sungura kwenye maficho yake. Akaanza kumkimbiza. Baada ya kukimbizana kwa muda mrefu, Mbwa alishindwa kumkamata kutokana na Sungura kumpiga chenga lukuki za maudhi. Akaamua kusimama.

Kundi la Mbuzi lilikuwapo mahali pale na walishuhudia kinagaubaga sakata hilo. Ikawa burudani kwao kwani mioyoni walikuwa wakimshabikia Sungura, na hawakupenda akamatwe na kuuawa. Walipomwona Mbwa akisimama kabla ya kutimiza azma yake ya kumkamata Sungura walimcheka na kumdhihaki sana,
wakimwambia “yule Sungura mdogo ndiye mkimbiaji hodari kuliko wewe Mbwa mkubwa!?”
Mbwa akawajibu, “shida ni kuwa hamjang’amua tofauti kati yetu: Mie nilikuwa nikikimbia ili tu nipate mlo wa jioni, wakati yeye alikimbia ili aokoe maisha yake.”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu