Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

HADITHI YA NYANI NA WANAWE MAPACHA

Ilisemekana wakati fulani kuwa Nyani mmoja alikuwa akizaa watoto wawili mapacha katika kila mzao wake. Na alikuwa na kasumba ya kumpenda na kumjali sana mtoto mmoja, yule mdogo, huku akimchukia na kutomjali kabisa yule mkubwa.

Ikatokea katika mzao wake mmoja kwamba yule mdogo aliyempenda na kumjali akasongwasongwa na kudhoofika kiafya na kimaadili kutokana na upendo wa mamaye uliopita kiasi, wakati yule mkubwa aliyechukiwa alipata mafundisho na kustawi licha ya kuishi maisha ya kutojaliwa na kuchukiwa na mama yake.

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu