Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA CHURA MTABIBU

Hapo zamani za kale kulikuwako Chura mkubwa.
Siku moja Chura huyo alijitokeza toka nyumbani kwake Kidimbwini Maguguni na kuwatangazia wanyama wote kwa kujitapa kwamba yeye ni mtabibu mjuzi, na ni mbobevu katika masuala ya tiba na dawa. Akatembea kifua mbele na kujigamba kuwa ana uwezo wa kutibu magonjwa ya aina zote, kwa jamii zote za wanyama!

Mbweha alijitokeza na kumuuliza, “Unathubutu vipi kujifanya tabibu wa wengine, ilhali unashindwa kujitibu mwenyewe ulemavu wako wa mwendo na makunyanzi ya ngozi!?”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3…………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu