Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

KISA CHA SUNGURA NA SIMBA

Hapo zamani za kale kulikuwako mkutano mkuu wa wanyama kila baada ya miaka mitatu, ambapo wanyama wote walipata fursa ya kutoa michango ya mawazo ili kuboresha kanuni na namna ya maisha yao kama jamii moja.

Siku moja, wakiwa katika mkutano kama huo, Sungura walitoa mawaidha kwa hisia kali sana, rai yao ikiwa ni kutaka wanyama wote wawe na haki sawa.

Tunataka haki sawa kwa wanyama wote, wakubwa kwa wadogo, wala nyama kwa wala nyasi…”

Simba ambaye alikuwa ndiye mwenyekiti wa mkutano akawajibu: “maneno yenu, enyi Sungura! ni mazuri sana; ila hayana makucha wala meno kama tuliyonayo sisi.”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu