Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

KISA CHA MWANAFALSAFA, MCHWA NA MEKYURI

Hapo zamani za kale, Mwanafalsafa mmoja alikuwa na kawaida ya kwenda ufukweni mwa bahari kila siku nyakati za jioni, kujipumzisha na kutafakari. Ikatokea alasiri ya jumamosi moja, akiwa ufukweni kama ilivyo ada yake, alishuhudia kwa macho yake mashua ikipigwa na dhoruba kali na kuzama.
Mabaharia na abiria wote waliokuwamo chomboni walizama na kufa maji. 

Yule bwana alihuzunika sana, hata alifikia kulaani kwamba majaaliwa ya Mungu hayakuwa ya haki kwani kutokana na mtu mmoja tu ambaye alipaswa kufikwa na mauti siku ile, umati mkubwa uliangamizwa pamoja naye. “Iweje roho za watu wote wale ziangamizwe kwa ajili ya mtu mmoja tu ambaye alipaswa kufa leo?” alijiuliza akiinua mikono yake juu kama ishara ya lawama kwa Mungu.

Wakati akiendelea kutafakari mawazo yake hayo, mara akajikuta amezungukwa na jeshi zima la Mchwa, ambao kumbe alikuwa amesimama kando ya nyumba yao.
Mmojawapo kati ya mchwa waliompanda miguuni alimng’ata na kumsababishia maumivu makali sana.
Yule bwana alighadhibika na kuanza kuwapondaponda kwa miguu na kuwaua mchwa wote waliokuwapo karibu naye.

Mara Mekyuri alitokea, akamcharaza fimbo za maonyo yule Mwanafalsafa huku akisema, “uu nani wewe hata ukatoa hukumu juu ya matendo ya Mungu juu ya wanadamu, ilhali wewe mwenyewe unatenda vivyo hivyo kwa Mchwa?”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu