Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 16 Juni 2014

KISA CHA NYANI WACHEZA SHOO

Mwanamfalme aliagiza Nyani kadhaa wapewe mafunzo maalum ya kucheza shoo. Kwa  vile kwa asili Nyani ni waigaji wazuri sana wa matendo ya binadamu, walionyesha kuwa wanafunzi bora wenye kushika mafuzo haraka, na walipovishwa nguo na vinyago kichwani, walicheza vizuri sana hadi kulingana au kwazidi wacheza shoo binadamu. 

Kwenye matamasha maonyesho yao mara nyingi yalishangiliwa kwa vifijo na nderemo, hadi siku moja jamaa fulani mcheza shoo mwenye wivu, aliyepania kuwafanyia hila, alitoa mfukoni mwake karanga za maganda na kuzirusha jukwaani. 
Basi ikawa wale Nyani, baada ya kuona karanga wakasahau kazi yao ya kucheza na wakawa (na kweli walikuwa) Nyani badala ya Wachezashoo
Walivua vinyago vyao na kuchanachana nguo walizovikwa, wakagombania karanga. Hivyo onyesho hilo likaishia hapo huku hadhira ikicheka na kudhihaki.
***
Share:

Kisa cha Wavulana na Vyura


Watoto wavulana, wakiwa wanacheza kandokando ya bwawa, waliona Vyura kwenye maji wakaanza kuwarushia mawe huku wakifurahia mchezo wa kulenga shabaha. 
Waliwaua vyura kadhaa, hadi Chura mmoja jasiri, alipotokeza kichwa chake nje ya maji, na kuwaambia kwa uchungu: 
"Acheni, acheni, enyi vijana: huu ambao ni mchezo kwenu, kwetu sisi ni kifo."
Share:

Kisa cha Mbwa na Mbweha

Mbwa, katika pitapita zao waliikuta ngozi ya Simba, wakaanza kuing'ata na kuirarua vipande vipande kwa meno yao. 

Mbweha aliwaona, akawaambia, 
"Laiti kama Simba huyo angekuwa hai, basi bila shaka mngetambua ya kuwa makucha yake yana nguvu kuliko hata meno yenu."
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu