Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

HADITHI YA SEREMALA NA SANAMU YA MEKYURI

Kulikuwa na mtu mmoja fukara sana, kazi yake ni fundi Seremala. Ndani ya nyumba yake pamoja na vitu vingine, aliweka sanamu ya Mekyuri ambaye aliaminika kuwa ni mjumbe wa Mungu. 

Kila siku fukara huyo aliitolea sanamu ile sadaka, na kuiomba imbariki na kumfanya kuwa tajiri. Lakini fundi alizidi tu kuwa fukara siku hadi siku, zaidi na zaidi.
Mwishowe alighadhibika, akaamua kuishusha sanamu ile toka kwenye kiweko chake na kuibamiza ukutani kwa jazba.

Baada ya kichwa cha Sanamu hilo kung’oka, zikamiminika dhahabu chungu nzima, ambazo fundi Seremala alizizoa na kusema, “Ewaa, nadhani sanaa yako kwa ujumla ni ya mkanganyiko na isiyoeleweka; kwani nilipokupa heshima na kukunyenyekea sikupata mali kutoka kwako: ila sasa nimekutenda vibaya umenijazia dhahabu na utajiri tele.”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu