Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MAKSAI NA WACHINJA NG'OMBE

Maksai, hapo zamani za kale, waliazimia kufanya hila ya kuwashambulia ghafla na kuwaangamiza Wachinja ng’ombe wote, kwa kuwa walikuwa wanaendesha biashara inayoteketeza jamii yao. Azimio hilo lilipitishwa kwa wingi mkubwa wa kura na maandalizi ya utekelezaji wake yakaanza mara moja.
Siku ya siku ilipofika walikusanyika ili waweze kutekeleza azma hiyo ya mauaji ya kushtukiza. Walinoa pembe zao vizuri kujiandaa kwa mapambano. Hamasa ilikuwa kubwa, na vijana walichagizwa kukaa mstari wa mbele.
Lakini miongoni mwao kulikuwako Maksai mmoja ambaye alikuwa mzee sana kwa umri (na wingi wa mashamba aliyokwishalima katika maisha yake) akawaasa kwa kuwaambia: “Ni kweli, Wachinja ng’ombe hawa wanatuchinja na kutuua, lakini tusisahau kuwa wanafanya hivyo kwa ujuzi na taaluma ya hali ya juu, na hivyo hutuepusha na maumivu yasiyo ya lazima. Endapo tutawashambulia na kuwaangamiza, tutaangukia mikononi mwa wafanyabiashara wasio na ujuzi wa kuchinja, na tutaanza kuuawa kwa nyundo na mashoka, kwa mateso na maumivu makali. Itakuwa ni kifo mara mbili zaidi: kwani hakika nawaambieni, ingawa tutawaangamiza Wachinja Ng’ombe wote, bado binadamu wataendelea kuhitaji nyama ya ng’ombe daima.”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu