Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA AYALA NA MZABIBU

Ayala, baada ya kukimbizwa na kuandamwa na wawindaji toka mbali, alichoka sana na kujua sasa mwisho wake umefika. Wawindaji walipomkaribia alifanya hila, akachupa kuume na kujibanza kwenye mvungu wa majani makubwa ya
Mzabibu. Wawindani nao kwa haraka waliyokuwa nayo (na hulka ya kuwahi ni kupata) hawakuweza kuing’amua hila yake, wakampita palepale bila kumwona.
Baada ya muda mfupi, kwa kudhani kuwa hatari haipo tena, Ayala aliinuka na kuanza kuyanyofoa nyofoa yale majani ya Mzabibu. Mwindaji mmoja aliyekuwa nyuma ya wenzake alisikia kwa mbali ule mchakato wa majani, akageuka kuangalia nyuma walikotoka, akamwona yule Ayala chini ya Mzabibu. Akachomoa mshale, akauweka kwenye upinde, akapiga na kumchoma Ayala tumboni.
Ayala, wakati akitapatapa karibia kukata roho, alikoroma na kusema; “Nimepata tijara nistahiliyo, kwani sikupaswa kabisa kuyatendea vile majani ya Mzabibu ambao punde uliokoa maisha yangu.”
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu