Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MAJOGOO WAWILI NA MWEWE

Majogoo wawili walioishi kwenye zizi moja walianza kupigana wakigombea ukuu katika himaya yao. Mwishowe jogoo Mwekundu alimshinda jogoo Mweupe, ambaye alisalimu amri na kukimbia.
Jogoo Mweupe alienda kujificha kwenye kona ya mbali kwa unyonge, ilhali yule Mwekundu aliyeshinda alirukia juu ya ukuta, akapiga mbawa zake na kuwika kwa sauti kuu kama ishara ya kuwa yeye ndiye mkuu hakuna mwingine zaidi yake. Ghafla Mwewe aliyekuwa akipita juu alimwona akamkamata na kumbeba kwa makucha yake akaondoka naye.
Ndipo yule jogoo Mweupe aliyeshindwa na kujificha alitoka konani na kutawala zizi akiwa huru asiye na mpinzani.

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu