Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 30 Desemba 2013

KISA CHA SIMBA NA PANYA

Siku moja mfalme Simba akiwa amejipumzisha kivulini, alipitiwa na usingizi. Panya mtukutu alimsogelea na kuanza kuchezacheza juu yake; hali ambayo ilimfanya aamke mara moja. Alipoamka, Simba alimkamata Panya kwa kumkandamiza na guu lake kubwa, tayari kwa kumla.

Naomba unisamehe, ee Mfalme,” Panya alilia na kuomba: “nisamehe kwa sasa na sitosahau kamwe: huwezi kujua pengine ipo siku mimi pia ninaweza kulipa wema wako kwa kukusaidia!.”

Simba aliguswa sana na maneno ya Panya kwamba eti huenda ipo siku akamsaidia yeye Simba, mnyama mkubwa ambaye ni mfalme wa wanyama wote. Aliinua mguu wake na kumwacha aende zake.

Siku moja Simba alinaswa kwenye mtego wa Binadamu, na wawindaji walipomkuta walipanga kumpeleka kwa Mfalme wao kama zawadi akiwa hai vilevile. Walimfunga kwenye mti kwa kamba kisha wakaondoka kwenda kutafuta usafiri wa kumbebea.

Punde ikatokea yule Panya alipita maeneo yale, na alipomwona Simba yupo katika hali ile ya taharuki, majonzi na hofu ya kuuawa, alienda pale mtini na kuzikatakata kwa meno yake makali kamba zile zilizomfunga Mfalme wa wanyama wote.
Si nilikwambia,? unaona sasa…” alisema Panya.

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu