Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Alhamisi, 30 Januari 2014

HADITHI YA BIBI KIZEE NA CHUPA YA MVINYO

Bibi kizee aliokota chupa tupu ya mvinyo ambayo alitambua kuwa siku nyingi zilizopita ilijaa mvinyo. Ila alishangaa kuona kuwa hadi wakati huo ilikuwa ikitoa harufu mzuri ya kinywaji hicho.

Kwa uchu, aliisogeza chupa hiyo puani na kuvuta harufu yake, akaitazama, kisha akarudia kuinusa mara kadhaa na kusema kwa husuda,
Oo… kinywaji murua kabisa! Yamkini huu ulikuwa Mvinyo maridadi kwelikweli, kwa maana umeacha kwenye chupa hii harufu nzuri sana ya manukato!”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu