Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA POPO, NDEGE NA WANYAMA

Hapo zamani za kale kulitokea mgogoro mkubwa sana kati ya Ndege na Wanyama, na vita kati yao ilinukia. Ilionekana kana kwamba juhudi zote za mapatano ziligonga mwamba. Wakati majeshi hayo mawili yakijikusanya kujiandaa kwa mapigano ya umwagaji damu, Popo alisita kuchagua upande wa kujiunga nao kivita.
Jeshi la Ndege lilipita karibu na kitulio chake na kumwambia; “Twende nasi vitani ee Popo ndege mwenzetu.”
Popo alikataa na kusema, “Mimi ni mnyama. Wala si ndege kama ninyi”
Baadaye jeshi la Wanyama nalo lilipita chini ya kitulio chake, walipomwona walimwita na kumwambia; “Twende nasi vitani ee Popo myama mwenzetu.” Popo alikataa tena na kujibu, “Mimi ni Ndege. Wala si mnyama kama ninyi.”
Basi kukawa na ngurumo za kutisha za wanyama shupavu kama vile simba duma na tembo; na ndege shupavu kama tai na furukombe. Anga lote lilijaa vitisho na harufu ya damu. Majike wenye ndama na majike wenye makinda walihisi kiyama chao kimefika.
Kwa bahati sana, katika dakika za mwisho mwisho kuelekea vita, muafaka ulifikiwa kati ya pande mbili hizo na vita vikaepukwa. Kukawa na amani badala ya mapigano. Kuona hivyo, Popo naye alitamani kuwa sehemu ya shamrashamra hizo. Alikwenda kwa Ndege akitaka kujiunga nao katika furaha na cherekochereko za kushangilia amani, wakamfukuza.
Akaamua kuondoka akaenda kwa wanyama huku akitabasamu na kutegemea kushiriki nao furaha ile ya amani. Nao walimfukuza kwa hasira hata akalazimika kukimbia wasije wakamdhuru kwa kumjeruhi au kumtoa roho kabisa.
Ah,” Popo alijisemea kimoyomoyo, “sasa nimeng’amua,”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………


Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu