Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumanne, 31 Desemba 2013

HADITHI YA MTOTO NA MBWA MWITU

Mtoto mmoja, akiwa anarudi peke yake kutoka machungani wakati wa jioni, alipita katikati ya kichaka ambako alikutana na Mbwa mwitu. Kumbe yule Mbwa mwitu alikuwa na njaa na alijua kuwa mtoto kama yule angetosha kabisa kwa chakula cha jioni kwake na kwa familia yake ya watoto wanne kule pangoni. Alianza kumnyemelea akimmezea mate kwa uchu. Yule...
Share:

Jumatatu, 30 Desemba 2013

KISA CHA SIMBA NA PANYA

Siku moja mfalme Simba akiwa amejipumzisha kivulini, alipitiwa na usingizi. Panya mtukutu alimsogelea na kuanza kuchezacheza juu yake; hali ambayo ilimfanya aamke mara moja. Alipoamka, Simba alimkamata Panya kwa kumkandamiza na guu lake kubwa, tayari kwa kumla. “Naomba unisamehe, ee Mfalme,” Panya alilia na kuomba: “nisamehe kwa sasa na sitosahau...
Share:

HADITHI YA SEREMALA NA SANAMU YA MEKYURI

Kulikuwa na mtu mmoja fukara sana, kazi yake ni fundi Seremala. Ndani ya nyumba yake pamoja na vitu vingine, aliweka sanamu ya Mekyuri ambaye aliaminika kuwa ni mjumbe wa Mungu.  Kila siku fukara huyo aliitolea sanamu ile sadaka, na kuiomba imbariki na kumfanya kuwa tajiri. Lakini fundi alizidi tu kuwa fukara siku hadi siku, zaidi na zaidi. Mwishowe alighadhibika,...
Share:

HADITHI YA MBWEHA NA PAKA

Mbweha alikuwa akijigamba mbele ya Paka kuwa yeye ana mbinu nyingi sana za kuwakwepa maadui zake. “Nina fuko zima la mbinu na ujanja,” alisema, “ambalo lina mamia ya njia za kujiepusha na maadui zangu wakati wa hatari.” “Mimi ninayo mbinu moja tu,” alisema Paka; “lakini ninaiamini, na inanifaa hiyo hiyo.” Wakiongea maneno hayo, punde wakasikia...
Share:

KISA CHA SUNGURA NA SIMBA

Hapo zamani za kale kulikuwako mkutano mkuu wa wanyama kila baada ya miaka mitatu, ambapo wanyama wote walipata fursa ya kutoa michango ya mawazo ili kuboresha kanuni na namna ya maisha yao kama jamii moja. Siku moja, wakiwa katika mkutano kama huo, Sungura walitoa mawaidha kwa hisia kali sana, rai yao ikiwa ni kutaka wanyama wote wawe na haki...
Share:

HADITHI YA SIMBA NA SUNGURA

Simba mwenye njaa, katika pitapita zake za kuwinda, alimkuta Sungura akiwa amelala fofofo. Alishusha pumzi, akatabasamu na kumshukuru sana Mungu kwa ukarimu wake wa kutambua taabiko lake na kumtunuku chakula pasi na haja ya kukitolea jasho. Taratibu alimsogelea Sungura ili asije akamwamsha, akalala yeye… Alipoinua miguu yake kutaka kumkamata,...
Share:

HADITHI YA MTU NA MTI

Mtu mmoja alikwenda kichakani huku akiwa na shoka mikononi kwake, na kuiomba Miti kwa unyenyekevu ili iweze kumpa tawi moja tu dogo ambalo alisema alikuwa na kazi nalo fulani. Miti ile ilikuwa na tabia njema, ikampa moja ya matawi yake. Kumbe yule mtu alikuwa akihitaji mpini wa shoka lake. Kwa kutumia tawi lile alilopewa akakarabati shoka lake...
Share:

HADITHI YA NYANI NA WANAWE MAPACHA

Ilisemekana wakati fulani kuwa Nyani mmoja alikuwa akizaa watoto wawili mapacha katika kila mzao wake. Na alikuwa na kasumba ya kumpenda na kumjali sana mtoto mmoja, yule mdogo, huku akimchukia na kutomjali kabisa yule mkubwa. Ikatokea katika mzao wake mmoja kwamba yule mdogo aliyempenda na kumjali akasongwasongwa na kudhoofika kiafya na kimaadili...
Share:

KISA CHA SIMBA, MBWA MWITU NA MBWEHA

Simba, kutokana na uzee wake, alilala akiwa hoi mgonjwa kwenye pango lake.  Wanyama wote wa mwituni walikwenda kumwona na kumsalimu mfalme wao, isipokuwa Mbweha. Kwahiyo Mbwa mwitu, ambaye walikuwa na uhasama wa jadi na Mbweha, aliwaza kuwa huo ulikuwa ni wasaa mzuri sana wa kumkomoa. Akabuni hila ya kutoa mashtaka kwa Mfalme Simba kwamba...
Share:

KISA CHA MWANAFALSAFA, MCHWA NA MEKYURI

Hapo zamani za kale, Mwanafalsafa mmoja alikuwa na kawaida ya kwenda ufukweni mwa bahari kila siku nyakati za jioni, kujipumzisha na kutafakari. Ikatokea alasiri ya jumamosi moja, akiwa ufukweni kama ilivyo ada yake, alishuhudia kwa macho yake mashua ikipigwa na dhoruba kali na kuzama. Mabaharia na abiria wote waliokuwamo chomboni walizama...
Share:

Jumatatu, 23 Desemba 2013

KISA CHA MBWEHA, JOGOO NA MBWA

Kulitokea usiku mmoja wa mbalamwezi Mbweha alikuwa akizungukazunguka kwa mawindo kwenye shamba la Mkulima mwenye mifugo, ambapo aliliona Jimbi moja limesimama juu kabisa asipoweza kufikia likiwika kwa sauti ya juu. “Habari njema, habari njema!” Mbweha alipaza sauti kwa hila. “Nijuze, ni ipi habari hiyo njema?” Jimbi lilijibu. “Mfalme Simba...
Share:

KISA CHA MWANAMFALME NA PICHA YA SIMBA

Hapo zamani kulikuwako Mfalme, ambaye alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume, kijana aliyependa sana mazoezi ya sanaa za mapigano. Kila siku alijichanganya na vijana wa rika lake katika mazoezi na michezo. Na awapo nyumbani alipendwa sana na wazazi wake, hasa baba yake. Siku moja Mfalme akiwa usingizini aliota ndoto. Na katika ndoto hiyo alipewa onyo...
Share:

KISA CHA KIJANA NA UPUPU

Hapo zamani kulikuwa na Kijana mmoja mtukutu ambaye alipenda sana kuchezea mimea na wadudu. Siku moja akiwa kwenye kichaka jirani na nyumbani kwake, aligusa Upupu kwa mkono wake wa kuume, nao ukaanza kumwasha. Ukamletea karaha na maumivu makali. Akaamua kukimbilia nyumbani kwake haraka huku akiendelea kujikuna na machozi yakimlengalenga. Alimfuata...
Share:

KISA CHA SUNGURA NA MBWEHA

Hapo zamani za kale Sungura walianzisha vita na Tai. Mapambano yalianza na kila upande ukijigamba na kudhani ulikuwa na uwezo wa kumshinda mwenzie. Vita vilipopamba moto, Sungura walihisi kuzidiwa. Baada ya vikao na mashauriano ya majemedari, walikubaliana kutuma maombi kwa Mbweha ili waje kama mamluki kuwasaidia kupambana na jeshi shupavu la...
Share:

KISA CHA MAJOGOO WAWILI NA MWEWE

Majogoo wawili walioishi kwenye zizi moja walianza kupigana wakigombea ukuu katika himaya yao. Mwishowe jogoo Mwekundu alimshinda jogoo Mweupe, ambaye alisalimu amri na kukimbia. Jogoo Mweupe alienda kujificha kwenye kona ya mbali kwa unyonge, ilhali yule Mwekundu aliyeshinda alirukia juu ya ukuta, akapiga mbawa zake na kuwika kwa sauti kuu kama...
Share:

KISA CHA CHURA MTABIBU

Hapo zamani za kale kulikuwako Chura mkubwa. Siku moja Chura huyo alijitokeza toka nyumbani kwake Kidimbwini Maguguni na kuwatangazia wanyama wote kwa kujitapa kwamba yeye ni mtabibu mjuzi, na ni mbobevu katika masuala ya tiba na dawa. Akatembea kifua mbele na kujigamba kuwa ana uwezo wa kutibu magonjwa ya aina zote, kwa jamii zote za wanyama! Mbweha...
Share:

KISA CHA POPO, NDEGE NA WANYAMA

Hapo zamani za kale kulitokea mgogoro mkubwa sana kati ya Ndege na Wanyama, na vita kati yao ilinukia. Ilionekana kana kwamba juhudi zote za mapatano ziligonga mwamba. Wakati majeshi hayo mawili yakijikusanya kujiandaa kwa mapigano ya umwagaji damu, Popo alisita kuchagua upande wa kujiunga nao kivita. Jeshi la Ndege lilipita karibu na kitulio chake...
Share:

KISA CHA KIJANA MWINDA SENENE

Kijana mmoja mdogo alikuwa akidaka Senene kwenye majani yaliyomea kando ya shamba lao. Ilikuwa ni mapema wakati wa asubuhi, hata umande ungali haujavukizwa. Baada ya nusu saa tu alifanikiwa kuwadaka Senene wengi sana. Wakati akijiandaa kurudi nyumbani, alitupa macho huku na huko na kumwona Nge akiwa amejipachika katikati ya majani mawili. Basi yule...
Share:

KISA CHA SUNGURA NA VYURA

Sungura walikuwa wakionewa sana na wanyama wengine kwa kupigwa, kuwindwa na kuliwa, kiasi kwamba hawakujua wakimbilie wapi. Ikawa wanaishi maisha ya karaha mno na kila walipomwona mnyama yeyote akiwakaribia, walilazimika kutimua mbio kwa woga. Siku moja wakaliona kundi la Farasi pori walio katika hali ya taharuki wakikimbia na kuwaelekea wao. Walihamaki...
Share:

KISA CHA SIMBA NA PAPA

Siku moja Simba alikuwa akirandaranda ufukweni mwa bahari, akamwona Papa akichomoza kichwa chake juu ya uso wa bahari katikati ya mawimbi. Alizama na kuibuka tena… akazama na kuibuka tena… Simba alivutiwa naye na kumwona kuwa anafaa kuwa rafiki kwani ni mkubwa na mwenye nguvu kama yeye. Alimwita karibu naye akasogea. Baada ya kusalimiana Simba...
Share:

KISA CHA MBWEHA NA MBU

Siku moja, baada ya kutembea kwa muda mrefu, Mbweha aliukuta mto mdogo wenye kina kifupi cha maji. Maji yalikuwa masafi na maangavu kabisa na mandhari ya bonde lile kwa ujumla ilikuwa ya kuvutia kutokana na uoto na magugu yaliyonawiri vizuri pembezoni. Akayatamani maji kwa uzuri wake japo hakuwa na kiu kabla, akayanywa, kisha akatulia kidogo kwa tafakuri. Hapohapo akapata...
Share:

KISA CHA SUNGURA NA MBWA

Katika pitapita zake za mawindo, Mbwa alimvumbua Sungura kwenye maficho yake. Akaanza kumkimbiza. Baada ya kukimbizana kwa muda mrefu, Mbwa alishindwa kumkamata kutokana na Sungura kumpiga chenga lukuki za maudhi. Akaamua kusimama. Kundi la Mbuzi lilikuwapo mahali pale na walishuhudia kinagaubaga sakata hilo. Ikawa burudani kwao kwani mioyoni...
Share:

KISA CHA MBUZI NA MCHUNGAJI

Mchunga Mbuzi alihangaika kumrudisha Mbuzi mmoja aliyetoka kundini na kuingia kwenye shamba la jirani. Alipiga mbinja na kupuliza baragumu bila ya mafanikio; yule Mbuzi alimbeza na kuidharau miito yote. Mwishowe Mchunga Mbuzi aliudhika na kumrushia jiwe kwa nguvu, likamvunja pembe moja. Kuona vile Mchunga Mbuzi alipagawa kwa...
Share:

KISA CHA BABU KIZEE NA KIFO

Babu kizee mmoja aliajiriwa kufanya kazi ya kukata magogo ya miti msituni. Siku moja akiwa anarejea nyumbani jioni alibebeshwa mzigo wa kuni aupeleke mjini ukauzwe. Mzigo ule ulikuwa mzito sana kwake. Baada ya mwendo wa kitambo kirefu alichoka akawa hoi kabisa. Alisononeka kwa ufukara wake unaopelekea apate mateso ya kufanya kazi mzito mchana kutwa,...
Share:

KISA CHA AYALA NA MZABIBU

Ayala, baada ya kukimbizwa na kuandamwa na wawindaji toka mbali, alichoka sana na kujua sasa mwisho wake umefika. Wawindaji walipomkaribia alifanya hila, akachupa kuume na kujibanza kwenye mvungu wa majani makubwa ya Mzabibu. Wawindani nao kwa haraka waliyokuwa nayo (na hulka ya kuwahi ni kupata) hawakuweza kuing’amua hila yake, wakampita palepale...
Share:

KISA CHA MAKSAI NA WACHINJA NG'OMBE

Maksai, hapo zamani za kale, waliazimia kufanya hila ya kuwashambulia ghafla na kuwaangamiza Wachinja ng’ombe wote, kwa kuwa walikuwa wanaendesha biashara inayoteketeza jamii yao. Azimio hilo lilipitishwa kwa wingi mkubwa wa kura na maandalizi ya utekelezaji wake yakaanza mara moja. Siku ya siku ilipofika walikusanyika ili waweze kutekeleza azma...
Share:

Jumamosi, 21 Desemba 2013

KISA CHA MJAKAZI NA NYOKA

Hapo zamani za kale, kulikuwapo Nyoka mkubwa mwenye sumu kali, ambaye aliweka makazi yake kwenye shimo pembezoni mwa baraza ya nyumba ya Mjakazi mmoja. Siku moja usiku wa manane yule Nyoka alimng’ata mtoto mchanga wa Mjakazi, mwili wake ukabadilika rangi kuwa mweusi tii, akafa. Kukawa msiba na simanzi isiyo kifani. Wakati akiomboleza kifo cha...
Share:

KISA CHA NGURUWE, KONDOO NA MBUZI

Nguruwe mmoja mdogo alikuwa amefungiwa kwenye uzio wa miti. Mbuzi na Kondoo pia walifungwa pamoja naye. Siku moja Mchungaji wao alikuja na kumkamata yule Nguruwe, ambaye aliguna na kuanza kupiga kelele na kufurukuta. Mbuzi na Kondoo walimlalamikia Nguruwe kwa kelele zake za kilio na purukushani, wakasema kwa kejeli, “Mara kwa mara Mchungaji...
Share:

KISA CHA MVUVI NA SAMAKI MDOGO

Ilitokea siku moja kuwa, Mvuvi, baada ya kuhangaika kwenye kazi yake ya kuvua kutwa nzima, aliambulia kukamata Samaki mmoja tu mdogo. Yule Samaki akamwambia Mvuvi kwa kumbembeleza; “Tafadhali niachie ee bwana,” alilalamika. “Mimi bado ni mdogo sana, sijafikia rika ya kuliwa nawe kwa sasa. Ukinihurumia na kunirudisha mtoni, nitakua haraka, na ndipo...
Share:

KISA CHA MWANAKONDOO NA MBWA MWITU

Mbwa mwitu alimkimbiza Mwanakondoo, ambaye ili kujiokoa alikimbilia ndani ya hekalu moja la ibada. Mbwa mwitu hakuweza kuingia hekaluni, badala yake alisimama nje akapaza sauti kumwita akimwambia, “Ni heri uje kwangu, maana humo ulimokimbilia Padre akikukamata atakuchinja na kukufanya dhabihu.” Mwanakondoo akamjibu, “Ni heri nitolewe kafara ndani ya...
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts