Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Jumamosi, 31 Mei 2014

KISA CHA NYIGU NA NYOKA

Nyigu alitua kwenye kichwa cha Nyoka na kuanza kumng’ata mfululizo, akimjeruhi vibaya kwa lengo la kutaka kumwua.  Nyoka, akiwa katika maumivu makali asijue namna ya kujiokoa na adui yake huyo, mara akaona mkokoteni uliojazwa magogo ya miti ukipita.  Basi kwa...
Share:

KISA CHA MITUNGI MIWILI

Mitungi miwili iliachwa kwenye ukingo wa mto, mmoja wa chuma, na mwingine wa udongo.  Baada ya mvua kubwa kunyesha mbali mto utokako ndipo maji ya mto yalipoongezeka na hatimaye mitungi yote ilisombwa ikaelea kufuata mkondo.  Basi ule mtungi wa udongo ukawa unafanya...
Share:

Ijumaa, 30 Mei 2014

KISA CHA MAADUI WAWILI

Jamaa wawili, ambao walikuwa ni maadui wa kufa na kupona, walijikuta wakisafiri katika merikebu moja. Wakiwa wamepania kukaa mbalimbali kadri iwezekanavyo, mmoja alienda kukaa nyuma kabisa na  mwingine mbele kabisa kwenye ncha ya mwisho ya merikebu.  Mara kukapiga dhoruba kali na mawimbi yakaanza kukipeleka chombo mrama, na kilipokuwa...
Share:

KISA CHA PANYA WA MJINI NA PANYA PORI

Panya Pori alimwalika panya wa mjini, ambaye ni rafiki yake kipenzi, amtembelee kwake aje ajionee maisha ya porini. Wakiwa kwenye uwanda wazi wa mashamba, wakila mabaki ya nafaka na mizizi ya miti iliyong’oka, Panya wa Mjini alimwambia rafiki yake,   “Huku shamba...
Share:

KISA CHA MBWA WAWILI

Kulitokea bwana mmoja ambaye alifuga mbwa wawili:  Mbwa mwindaji, ambaye alimfundisha kumsaidia katika kazi zake za uwindaji, na Mbwa mlinzi, aliyemfundisha kulinda nyumba.  Kila aliporejea nyumbani kutoka mawindoni, alikuwa akimpa yule Mbwa wa nyumbani minofu...
Share:

Alhamisi, 22 Mei 2014

Kisa cha Bwana Mzalendo mwenye Kipawa

Baada ya kufanikiwa kupewa nafasi ya kusikilizwa na mfalme na baraza lake la washauri, Mzalendo mwenye kipaji alitoa karatasi mfukoni mwake, akasema:  ::soma zaid...
Share:

Jumapili, 18 Mei 2014

KISA CHA TAI, PAKA NA NGURUWE PORI

Kulitokea Tai mmoja ambaye alijenga kiota chake juu ya mti mkubwa; Paka naye, baada ya kuona kuna shimo linalomfaa, alihamia na kuanza kuishi katikati ya shina la mti ule ule; na Nguruwe pia, akiwa na vitoto vyake, akaweka makazi kwenye shimo lililopo wazi chini ya mti ule.  Basi...
Share:

KISA CHA MARAFIKI WAWILI NA DUBU

Marafiki wawili walikuwa wakisafiri pamoja kupitia vichakani, mara akatokea dubu mkubwa na kuanza kuwakimbiza. Katika harakati za kutaka kujiokoa walikimbia na ikawa mmoja kati yao alikuwa mbele na mwingine nyuma yake.  Basi yule wa mbele iliwahi kulishika tawi la...
Share:

Jumamosi, 17 Mei 2014

KISA CHA BAHILI NA DHAHABU ZAKE

Bwana mmoja bahili aliuza vitu vyake vyote alivyonavyo na kununua sarafu za dhahabu, ambazo alichimba shimo na kuzifukia chini kando ya ukuta wa zamani na kuwa anakwenda kuziangalia kila siku. Mmoja wa wafanyakazi wake aligundua safari zake za mara kwa mara kwenda eneo lile...
Share:

KISA CHA MBWA NA MBWA MWITU

Mbwa-mwitu mmoja dhaifu alikuwa akikaribia kufa kwa njaa na mara kwa bahati akakutana na mbwa wa nyumbani ambaye alikuwa akipita.  "Ah, binamu," alisema mbwa "nilijua tu yatakukuta haya; kwamba maisha yako ya kutangatanga na yasiyo na uhakika ipo siku yatakuangamiza....
Share:

KISA CHA MBWA NA SUNGURA

Mbwa mwindaji alimvumbua Sungura kwenye mafukutu juu ya kilima na kuanza kumkimbiza kwa kitambo, wakati fulani alimkaribia na kung'ata kwa nguvu kwa meno yake makali kana kwamba ataka kumuua, na mara nyingine alimkumbatia kana kwamba anacheza na mbwa mwenzake.  Yule...
Share:

KISA CHA MZEE KIPARA NA MBUNG'O

Mbung'o alitua kichwani kwa Mzee mmoja na kumng'ata kwenye sehemu yenye kipara, ambapo yule Mzee kwa kutaka kumwangamiza Mbung'o alijipiga kofi pwaaa!  Yule mbung'o alifanikiwa kukwepa na aliondoka akisema kwa dhihaka,  "Ulipanga kulipiza kisasa, hata kwa kuua,...
Share:

KISA CHA MAMA NA MTETEA

Hapo zamani za kale kulikuwako mama mmoja ambaye alikuwa na kuku wake mtetea aliyetaga yai moja kila siku.  Kila wakati yule mama alifikiri na kujiuliza atawezaje kupata mayai mawili kwa siku badala ya moja, na mwishowe, ili kutimiza azma yake, akaamua kuanza kumlisha...
Share:

KISA CHA MBWEHA ALIYEKATWA MKIA

Hapo zamaini za kale, kulitokea Mbweha mmoja mjanja. Siku moja kwenye pitapita zake kwa bahati mbaya alinaswa mtegoni, na katika kuhangaika alifanikiwa kujinasua, ila alikatika mkia ukabakia kipisi kifupi tu. Siku za mwanzo mwanzo aliona aibu kujionyesha ulemavu wake wa kutokuwa na mkia kwa mbweha wenzake. Baadaye akaamua kujibaraguza na kufanya...
Share:

Jumatano, 7 Mei 2014

KISA CHA MBWEHA, MBWA MWITU NA NYANI

Mbwa mwitu alimshutumu  vikali Mbweha kwa kumwibia, ila Mbweha alikana katukatu kwamba hakutenda kosa hilo. Baada ya kuzozana kwa muda, wakampelekea Nyani shauri hilo ili atoe hukumu na kumaliza mgogoro baina yao.  Basi baada ya kila mmoja wao kupewa nafasi ya kujieleza kwa kina, Nyani akatangaza hukumu ifuatayo:  "Siamini katu...
Share:

KISA CHA WASAFIRI WAWILI NA SHOKA

Jamaa wawili walikuwa wakisafiri pamoja. Wakiwa njiani mmoja wao aliokota shoka zuri lililokuwa limelazwa kando ya njia, akalichukua na kusema,  "Nimeokota shoka."  "Hapana rafiki yangu," mwenzake alimjibu, "usiseme 'Nimeokota' bali 'Tumeokota' shoka."  Basi...
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts