Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Ijumaa, 30 Mei 2014

KISA CHA MBWA WAWILI

Kulitokea bwana mmoja ambaye alifuga mbwa wawili: 
Mbwa mwindaji, ambaye alimfundisha kumsaidia katika kazi zake za uwindaji, na Mbwa mlinzi, aliyemfundisha kulinda nyumba. 

Kila aliporejea nyumbani kutoka mawindoni, alikuwa akimpa yule Mbwa wa nyumbani minofu mikubwa mikubwa ale. Mbwa mwindaji hakupendezwa na jambo lile na alishindwa kuvumilia, alimfuata mwenzie, akamwambia, 

“Ni mateso makubwa kufanya kazi ngumu kama nifanyayo mimi, ilhali wewe, ambaye husaidii lolote katika kuwinda, unajibarizi na kufaidi matunda ya jasho langu.” 

Mbwa wa nyumbani akamjibu, 
“Rafiki yangu, usinilaumu mimi bali umlaumu bwana wetu, ambaye hajanifundisha mimi kufanya kazi bali kuishi kwa kutegemea matunda ya kazi za wengine.”
***
Share:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu