Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Alhamisi, 30 Januari 2014

KISA CHA NG'OMBE NA CHURA

Ng’ombe Maksai alikwenda kunywa maji katika dimbwi ambalo lilikuwa na watoto wa chura. Watoto hao walizaliwa hapo na kwao hiyo ilikuwa ni maskani yao halali. Ila kwa wakati ule mama yao alikuwa ametoka, kaenda kuitembelea familia ya rafiki yake iliyokuwa na makazi kwenye dimbwi jingine upande wa pili wa kichaka.

Kwa bahati mbaya, Maksai alimkanyaga mtoto mmoja wa Chura na kumjeruhi vibaya, akafa. Punde mama yao akarejea toka matembezini na kubaini kuwa mmoja wa watoto wake hayupo dimbwini. Akawauliza wale nduguze kulikoni.

Mwenzetu amekufa, mama mpenzi;” alijibu mmoja wao kwa majonzi.
Kumetokea nini tena mbona niliwaacha wote wazima?” mama Chura alihoji.
Muda si mrefu uliopita mnyama mkubwa sana alikuja dimbwini akamkanyaga kwa kwato zake kubwa na kumuua.” walimjibu.

Chura alihamaki mno, akaanza kuvuta pumzi na kujitunisha kwa hasira, akahoji, “iwapo baradhuli huyo alikuwa mkubwa kiasi hicho kwa umbo,”
Ee mama yetu mpendwa, acha kujijaza upepo na kujitunisha” mtoto wake mmoja alimkatisha, “na wala usighadhibike kiasi hicho; kwani hakika nakuambia, utaanza kupasuka mwili kabla hujafanikiwa kuiga ukubwa wa dhalimu yule.”

Hadithi hii inatufundisha nini?
1……………………………………………………………………………………………………………………
2……………………………………………………………………………………………………………………
3……………………………………………………………………………………………………………………
Taja methali, nahau au msemo wa Kiswahili wenye maana inayofanana na maudhui ya hadithi hii;
………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………

Share:

Maoni 2 :

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Popular Posts

Kumbukumbu la Blogu