Bibi kizee
aliokota chupa tupu ya mvinyo ambayo alitambua kuwa siku nyingi
zilizopita ilijaa mvinyo. Ila alishangaa kuona kuwa hadi wakati huo
ilikuwa ikitoa harufu mzuri ya kinywaji hicho.
Kwa uchu,
aliisogeza chupa hiyo puani na kuvuta harufu yake, akaitazama, kisha
akarudia kuinusa mara kadhaa na kusema kwa husuda,
“Oo… kinywaji murua kabisa!...
Alhamisi, 30 Januari 2014
KISA CHA NG'OMBE NA CHURA
Ng’ombe
Maksai alikwenda kunywa maji katika dimbwi ambalo lilikuwa na watoto
wa chura. Watoto hao walizaliwa hapo na kwao hiyo ilikuwa ni maskani
yao halali. Ila kwa wakati ule mama yao alikuwa ametoka, kaenda
kuitembelea familia ya rafiki yake iliyokuwa na makazi kwenye dimbwi
jingine upande wa pili wa kichaka.
Kwa bahati
mbaya, Maksai alimkanyaga...
Alhamisi, 2 Januari 2014
HADITHI YA MBWEHA NA CHUI
Siku moja
mbweha na chui walizozana kuhusu nani kati yao alikuwa mzuri kuliko
mwenzake. Chui alijinadi kwa kumwonyesha mbweha moja baada ya jingine
madoa yaliyoipamba na kuipendezesha ngozi yake. Na kweli ukimwangalia
Chui na madoa yake alionekana mzuri anayevutia.
Lakini mbweha
naye alimkatiza kwa kusema, “hivi ni nani mzuri kati yako wewe,...
KISA CHA MWANADAMU NA SIMBA

Mwanadamu na
Simba walikuwa wakisafiri pamoja kuelekea upande mwingine wa nchi.
Wakiwa safarini walianza kutambiana, kila mmoja akijigamba kuwa ni
mkuu na mwenye ushujaa na umahiri.
Wakati
wakiendelea kubishana, walipita mahali ambapo kulikuwa na sanamu
kubwa ya mawe ikimwonyesha...
KISA CHA MCHEKESHAJI NA MWANAKIJIJI
Hapo zamani
kulikuwepo mtu mmoja tajiri aliyeheshimika sana na watu wa jamii
yake. Bwana huyo alifungua majumba ya maonyesho ya sanaa na watu wote
waliruhusiwa kuingia bure. Wake kwa waume, watoto na wakubwa. Ikawa
baada ya kazi nyingi za kutwa za kujitafutia riziki, Wananchi
wakapata burudani na kufurahi pamoja.
Ila kwa kuwa
maonyesho yalifanyika...
HADITHI YA TAI NA MBWEHA
Tai
na Mbweha walikuwa marafiki wapenzi na hivyo walikubaliana kutoishi
mbalimbali. Wakautafuta mti mmoja mzuri. Tai akajenga kiota chake
kwenye matawi ya mti huo mkubwa, wakati Mbweha aliweka makazi yake
kwenye shimo chini ya mti huo huo. Miezi michache baadaye Mbweha
alizaa vitoto vinne.
Muda
si mrefu baada ya makubaliano yao ya kuishi jirani...
KISA CHA MUUAJI
Mtu mmoja
alimjeruhi mwenzie na kumuua. Ndugu na jamaa wa marehemu walianza
kumkimbiza wakiwa na silaha kwa minajili la kumuua kwa kisasi.
Yule muuaji
alikimbia kwa bidii kuu ili aokoe roho yake na hatimaye akafika
kwenye kingo ya mto Nile. Ng’ambo ya mto alimwona Simba na kwa woga
wake wa kuhofia kuuawa akaamua kukwea juu ya mti.
Kule...
HADITHI YA SIMBA, MBWEHA NA WANYAMA WENGINE
Siku moja
Simba alitangaza kuwa yu mgonjwa mahtuti na kwamba alikaribia kufa.
Hivyo alitoa tamko la kuwaalika Wanyama wote waende nyumbani kwake
kumwona na kusikia wosia wake wa mwisho na ushuhuda wa mambo kadha wa
kadha, na pia wapate busara za mfalme.
Hivyo Mbuzi
alienda kwenye pango alililoishi Mfalme Simba ili kumjulia hali.
Alisimama kwenye...