Hadithi za kale zenye mafundisho za Esopo zilizoandikwa zaidi ya miaka 3000 iliyopita. Zimetafsiriwa kwa Kiswahili na Issa S. Kanguni, chini ya shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Inventors and Techno-Thinkers Consortium (TITC). Tel; +255757242960

Tafuta katika Blogu Hii

Pages

Alhamisi, 30 Januari 2014

HADITHI YA BIBI KIZEE NA CHUPA YA MVINYO

Bibi kizee aliokota chupa tupu ya mvinyo ambayo alitambua kuwa siku nyingi zilizopita ilijaa mvinyo. Ila alishangaa kuona kuwa hadi wakati huo ilikuwa ikitoa harufu mzuri ya kinywaji hicho. Kwa uchu, aliisogeza chupa hiyo puani na kuvuta harufu yake, akaitazama, kisha akarudia kuinusa mara kadhaa na kusema kwa husuda, “Oo… kinywaji murua kabisa!...
Share:

KISA CHA NG'OMBE NA CHURA

Ng’ombe Maksai alikwenda kunywa maji katika dimbwi ambalo lilikuwa na watoto wa chura. Watoto hao walizaliwa hapo na kwao hiyo ilikuwa ni maskani yao halali. Ila kwa wakati ule mama yao alikuwa ametoka, kaenda kuitembelea familia ya rafiki yake iliyokuwa na makazi kwenye dimbwi jingine upande wa pili wa kichaka. Kwa bahati mbaya, Maksai alimkanyaga...
Share:

Alhamisi, 2 Januari 2014

HADITHI YA MBWEHA NA CHUI

Siku moja mbweha na chui walizozana kuhusu nani kati yao alikuwa mzuri kuliko mwenzake. Chui alijinadi kwa kumwonyesha mbweha moja baada ya jingine madoa yaliyoipamba na kuipendezesha ngozi yake. Na kweli ukimwangalia Chui na madoa yake alionekana mzuri anayevutia. Lakini mbweha naye alimkatiza kwa kusema, “hivi ni nani mzuri kati yako wewe,...
Share:

KISA CHA MWANADAMU NA SIMBA

Mwanadamu na Simba walikuwa wakisafiri pamoja kuelekea upande mwingine wa nchi. Wakiwa safarini walianza kutambiana, kila mmoja akijigamba kuwa ni mkuu na mwenye ushujaa na umahiri. Wakati wakiendelea kubishana, walipita mahali ambapo kulikuwa na sanamu kubwa ya mawe ikimwonyesha...
Share:

KISA CHA MCHEKESHAJI NA MWANAKIJIJI

Hapo zamani kulikuwepo mtu mmoja tajiri aliyeheshimika sana na watu wa jamii yake. Bwana huyo alifungua majumba ya maonyesho ya sanaa na watu wote waliruhusiwa kuingia bure. Wake kwa waume, watoto na wakubwa. Ikawa baada ya kazi nyingi za kutwa za kujitafutia riziki, Wananchi wakapata burudani na kufurahi pamoja. Ila kwa kuwa maonyesho yalifanyika...
Share:

HADITHI YA TAI NA MBWEHA

Tai na Mbweha walikuwa marafiki wapenzi na hivyo walikubaliana kutoishi mbalimbali. Wakautafuta mti mmoja mzuri. Tai akajenga kiota chake kwenye matawi ya mti huo mkubwa, wakati Mbweha aliweka makazi yake kwenye shimo chini ya mti huo huo. Miezi michache baadaye Mbweha alizaa vitoto vinne. Muda si mrefu baada ya makubaliano yao ya kuishi jirani...
Share:

KISA CHA MUUAJI

Mtu mmoja alimjeruhi mwenzie na kumuua. Ndugu na jamaa wa marehemu walianza kumkimbiza wakiwa na silaha kwa minajili la kumuua kwa kisasi. Yule muuaji alikimbia kwa bidii kuu ili aokoe roho yake na hatimaye akafika kwenye kingo ya mto Nile. Ng’ambo ya mto alimwona Simba na kwa woga wake wa kuhofia kuuawa akaamua kukwea juu ya mti.  Kule...
Share:

HADITHI YA SIMBA, MBWEHA NA WANYAMA WENGINE

Siku moja Simba alitangaza kuwa yu mgonjwa mahtuti na kwamba alikaribia kufa. Hivyo alitoa tamko la kuwaalika Wanyama wote waende nyumbani kwake kumwona na kusikia wosia wake wa mwisho na ushuhuda wa mambo kadha wa kadha, na pia wapate busara za mfalme. Hivyo Mbuzi alienda kwenye pango alililoishi Mfalme Simba ili kumjulia hali. Alisimama kwenye...
Share:

Live Traffic Feed

Blogroll

BTemplates.com

Inaendeshwa na Blogger.

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

183374

Popular Posts